Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Maalim Seif Sharif Hamad ameuagiza uongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo kuzuia matumizi ya jengo la Makumbusho kuu ya Zanzibar baada
ya kupata athari za kubomoka jana usiku.
Maalim Seif ametoa agizo hilo baada ya
kutembelea na kuangalia maharibiko yaliyotokea baada ya jengo hilo kubomoka
sehemu ya upande wa Ngome Kongwe na kusababisha hasara kubwa.
Hata hivyo Makamu wa Kwanza wa Rais
ameelezea haja ya kulifanyia matengenezo jengo hilo ili kutunza historia ya
Zanzibar na hifadhi ya Mji Mkongwe ambao ni urithi wa Kimataifa.
Akizungumzia hali hiyo, Waziri wa
Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Zanzibar Mhe. Said Ali Mbarouk amesema
jengo hilo limepata athari hiyo wakati likiendelea kufanyiwa
ukarabati.
Amesema baada ya kuona athari
zilizojitokeza hapo kabla, waliamua kulifanyia ukarabati kwa kuanza na hatua ya
uezekaji, lakini mvua zinazoendelea kunyesha zimekuwa zikipelekea jengo hilo
liendee kuvuja na kupelekea kubomoka sehemu hiyo.
Amesema kutokana na athari hiyo,
wameamua kuitisha kikao ili kutathmini hasara iliyopatikana na kutokana na
uharibifu huo.
Mhe. Mbarouk amefahamisha kuwa baada
ya kikao hicho watashauriana na washirika wa maendeleo wakiwemo mradi wa MACEMP
uliokuwa ukisaidia kulifanyia ukarabati jengo hilo pamoja na majengo mengine ya
kihistoria, ili waweze kuendeleza ukarabati huo.
Hassan Hamad (OMKR).
|
Home
»
»Unlabelled
» Maalim Seif azuwiya matumizi ya makumbusho mara baada ya kubomoka
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment