Viongozi mbali mbali wa vyama vya
siasa na serikali wameshiriki katika mazishi ya bibi Kisa Mohd ambaye ni mke wa
Mbunge wa Jimbo la Wawi (CUF) Mhe. Hamad Rashid Mohd.
Mazishi hayo yaliyofanyika nyumbani
kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya kisutu,
yaliongozwa na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda na Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad.
Viongozi wengine waliohudhuria ni
pamoja na Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman
Mbowe, Mwenyekiti wa UDP John Cheyo, Mwenyekiti wa ADC bw. Said Miraji na Spika
wa Bunge Mhe. Anne Makinda.
Mwili wa marehemu huyo ulisaliwa
katika msikiti Maamur ulioko maeneo ya Upanga na baadaye kupelekwa katika
makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi.
Marehemu bibi Kisa Mohd alifariki
Jumanne iliyopita baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Presha kwa muda mrefu, na
kuzikwa Alkhamis tarehe 29/11/2012.
Akizungumza katika mazishi hayo,
msemaji wa familia hiyo amewashukuru viongozi na wananchi waliojitokeza
kushirikiana nao katika msiba huo, na kwamba familia imepoteza mtu muhimu ambaye
pengo lake haliwezi kuzibika kwa kipindi kifupi.
Hassan Hamad,
OMKR.
|
Home
»
»Unlabelled
» Pole Mhe.Hamadi kwa msiba
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment