Muanzilishi wa  Mradi wa Taa zinazotumia mwanga wa Jua kutoka Kampuni ya Wakawaka ya Nchini Uholanzi Bwanan Maurits Groen akimkabidhi Taa inayotumia mwanga wa jua mmoja wa wananchi kadhaa wa Vijiji vya Matetema na Kichungwani ndani ya Jimbo la Kitope
Kampuni inayojishughulisha na mradi wa Umeme unaotumia Jua {Solar Energy } yenye Makao Makuu yake Nchini Uholanzi ya Wakawaka imetoa msaada wa Taa Mia Nne zinazotumia nguvu za mwanga wa jua kwa Vijiji viwili vya Matetema na Kichungwani vilivyomo ndani ya Jimbo la Kitope Wilaya ya Kaskazini B. 
Halfa ya ugawaji wa Taa hizo imesimamiwa na Mbunge wa Jimbo hilo Balozi Seif Ali Iddi  pamoja na Mkurugenzi Masoko wa Kampuni ya Wakawaka Bwana Bill Carney ambapo jumla ya Nyumba 86 za Kijiji cha Matetema na 160 za Kijiji cha Kichungwani zilipata mgao wa Taa moja kwa kila nyumba.  
 Jumla ya shilingi Milioni 25,000,000/-  zimetumika kutengenezea Taa hizo  mia Nne zitakazosaidia kupunguza matumizi makubwa  ya Taa za Vibatari zinazotumia Mafuta ambapo kila taa moja ina Thamani ya Shilingi  Sitini elfu {60,000/- }. 
 Akizungumza na Wananchi wa Vijiji hivyo vya Matetema na Kichungwani kwa  nyakati tofauti Muanzilishi wa Mradi huo wa Taa zinazotumia mwanga wa Jua kutoka Kampuni ya Wakawaka Bwana Maurits Groen alisema Kampuni yao imeamua kuanzisha mradi huo kwa lengo la kusaidia Jamii yenye kipato cha Chini katika Mataifa mbali mbali Duniani.Bwana Maurits alisema Jamii kubwa hasa katika Mataifa maskini zimekuwa zikitumia gharama kubwa kwa ununuzi wa mafuta kwa ajili ya matumizi ya Taa jambo ambalo linawaongezea mgizo wa matumizi wakati kipato chao ni hafifu. 
 Alisema pia yapo matatizo ya uchafuzi wa mazingira pamoja na ajali za mara kwa mara za moto zinazosababishwa na matumizi makubwa ya Taa za Vibatari ambazo huleta athari na wakati mwengine maafa kutuokana na Taa hizo.   Naye Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi aliipongeza Mampuni hiyo  ya Wakawaka ya Nchini Uholanzi kwa uamuzi wake wa kusaidia Wananchi wa Jimbo la Kitope katika kujipatia huduma za Taa zinazotumia mwanga wa Jua. 
 Balozi Seif ambaye pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema Taa hizo kwa kiasi kikubwa zitaweza kusaidia matumizi mbali mbali majumbani likiwemo lile muhimu la wanafunzi  kupata wasaa wa kudurumu masomo yao.Alisema kwa Vile Tanzania na Zanzibar kwa ujumla zimebahatika kuwa na kipindi kirefu cha Jua ndani ya mzunguuko wa mwaka wa miongo yake Taa hizo  zitakuwa na uwezo wa kutoa huduma kwa kadri ya lengo lililokusudiwa  la kuanzishwa kwa mradi huo.  
“ Haya ni maendeleo ya kuachana na Taa za Vibatari kwa vile tayari tumeshakuwa na Taa isiyohitaji mafuta ambayo ni gharama na yanachafua mazingira”. Alisema Balozi Seif. 
 Mradi huo wa Kampuni ya Wakawaka wa Taa  zinazotumia mwanga wa Jua ni   wa mwanzo kuingia ndani ya Bara la Afrika ukiwa  ni wa majaribio.  
 Mbunge huyo wa Jimbo la  Kitope  akiambatana na Ujumbe wa Uongozi wa Kampuni hiyo ya Wakawaka inayosimamia mradi wa Taa zinazotumia mwanga wa Jua walipata fursa ya Kuangaliwa Umeme unaotumia jua kwa baadhi ya Nyumba na Msikiti uliopo katika Kijiji hicho cha Kichungwani.  
Muanzilishi wa Mradi wa Taa hizo Bwana Maurits Groen alimueleza Balozi Seif kwamba Kampuni yake ina uwezo wa kila hali kutengeneza Vifaa vya Umeme unaotumia mwanga wa jua.
 Othman Khamis Ame  
 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 

0 comments:

 
Top