Busara Promotions inatoa taarifa ya tarehe ya tamasha la 10 la sauti za busara ambalo liataanza tarehe 14 – 17 februari 2013 katika ukumbi wa kihistoria wa ngome kongwe, Zanzibar.
Sauti za busara ni tukio la muziki la kila mwaka ndani ya afrika mashariki na kufahamika zaidi kama ‘tamasha rafiki katika sayari’. Katika toleo la mwakani litawaletea wanamuziki 200: zaidi ya vikundi 20 kutoka afrika mashariki na kwingineko vitafanya maonyesho yao ya moja kwa moja (live)
Ngome kongwe patafanyika maonyesho ya muziki kwa siku tatu mfululizo, ratiba kuu itaendelea  mpaka jumapili kwa maonyesho kuanzia saa 11 jioni mpaka saa 7 usiku.
Tamasha litaonyesha filamu za muziki wa kiafrika: Makala, video za muziki na matamasha, yote haya katika kuangazia uendeleza wa utajiri na mchanganyiko wa muziki wa afrika.
Sauti za Busara litaendelea na uendeshaji wa kongamano lijulikanalo kama Movers and Shaker kwa ajili ya wenyeji na wageni wataalam wa sanaa. Kongamano hili linatoa nafasi ya majadiliano, kubadilishana mawazo na uendelezaji wa mawazo ya ubunifu katika ukanda wa afrika mashariki na kwingineko.
Si tu tamasha linafanya uandaaji maonyesho, jamii inahimizwa kuandaa matukio ya ziada ya busara. Hayo yakiwemo Ngoma za kiutamaduni, Maonyesho ya mavazi, mashindano ya ngalawa na maonyesho ya vikundi vikongwe vya taarab ambayo yanaandaliwa na wenyeji.
Ni miaka tisa sasa tangu tamasha lianzishwe rasmi mwaka 2004, Tamasha limefanikiwa kuwapandisha jukwaani wasanii mbalimbali akiwemo Samba Mapangala & Orchestra Virunga, Natacha Atlas, Didier Awadi, Bassekou Kouyate, Jagwa Music, Tumi & The Volume, Freddy Masamba, Thandiswa, Mlimani Pack Orchestra, Culture Music Club, Orchestra Poly Rythmo na wengineo wengi. Tamasha linafanya muziki wa moja kwa moja (Live).
Kuanzia mwezi wa nne wasanii wanaweza kufanya maombi ya moja kwa moja kupitia tovuti yetu ya Sauti za Busara. Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 30/7/2012. Tamasha linatafuta wasanii wanaochipukia na wakongwe ili mushiriki katika tamasha. Kitu cha muhimu ni maonyesho kufanyika moja kwa moja kwa asilimia mia (100% live) na hakika inaunganisha afrika.
Msanii anayetaka kutuma maombi kupitia tovuti yetu inabidi atembelee tovuti yetu ya www.busaramusic.org
Mwisho wa kupokea maombi ni 31/7/2012.
na akamilishe ujazaji wa fomu au kwa kupitia sanduku letu la posta kama ifuatavyo Busara Promotions, P O Box 3635, Stone Town, Zanzibar, Tanzania.

0 comments:

 
Top