Chama cha National League for Democracy(NLD) kinalaani vikali juu ya mfumo mzima wa utoa wa hukumu katika mahkama ya vileo mjini Zanzibar.
Aidha katika taarifa yao kwa vyombo vya habari mjini hapa chama hicho cha NLD kimeeleza kwamba hakiridhishwi hata kidogo na mfumo wa utoaji wa lesini za kuendeshea biashara hizo za pombe kwa kimeeleza kwamba kwa asilimia kubwa huwa zinaharibu mila, silka na desturi za kizanzibari
Mbali na hayo, chama hicho kimesema ipo haja kwa mahkama hiyo ya vileo kuangalia upya jinsi ya utoaji wa leseni hizo kwani mara nyingi baa zinazolalamikiwa zipo karibu na makaazi ya watu na nyumba za ibada

0 comments:

 
Top