Bendi iliyokuja kwa kasi na inayoendelea kutamba hapa nchini kwa sasa Skylight Band inatazamiwa kuwa kivutio kikubwa katika tamasha la filamu nchini ZIFF.

Bendi hiyo inayoongozwa na mwanadada Aneth Kushaba, AK 47 inajipanga kupiga shoo kali ya karne katika Tamasha hilo la 16 la filamu za kimataifa litakalofanyika ndani ya Ngome Kongwe mjini Zanzibar.

Akizungumzia ushiriki wao Aneth Kushaba alisema “Zanzibar patakuwa hapatoshi, tumefurahi kupata fursa ya kutumbuiza ZFF na tunasubiri kwa hamu kubwa kujitangaza kimataifa”.

Skylight inayoundwa na wanamuziki kama Sam Machozi, Jonicho Flower na wengine kibao pia kwa sasa inatamba na vibao kama Karolina, Wivu, Nasaka Dough, na wimbo wao mpya Mbeleko.

0 comments:

 
Top