Jukwaa la Wanawake Wajasiriamali Tanzania- TWENDE linatarajia kufanyika kuanzia tarehe 18 – 20 ya mwezi wa kumi 2012 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
TWENDE imekuwa ikifanyika kila mwaka kwa mwaka watatu sasa tangu kuanzishwa kwake mwaka 2010, lengo likiwa ni kuwaleta pamoja wanawake wajasiriamali wadogo, wakubwa na wale wanaochipukia ili kupata fursa ya kuuza, kuonesha na kujadili masuala ya biashara kwa ujumla.
Sambamba na hilo. TWENDE inalenga kusaidiana na serikali katika kutimiza malengo ya milenia likiwemo lengo namba moja ambalo linalenga kuondoa umasikini, namba tatu kutetea haki na fursa sawa kwa wanawake, lengo namba tano kuhamasisha afya ya uzazi  na lengo  namba nane, ambayo ni  kuendeleza uhusiano wa kudumu kwa ajili ya maendeleo ya jamii. Pia TWENDE inalenga Kukuza uzalishaji kwa wanawake wafanyabiashara na kukuza mgawanyiko wa masoko sambamba na muonekano wa wafanyabiashara wanawake katika jamii.
Kwa upande wa mwaka huu TWENDE inatarajia kuwashirikisha wanawake wajasiriamali wengi zaidi ambao wamekuwa wakifanya biashasha tofauti ili kuweza kupata fursa ya kubadilishana uzoefu na kuongeza ujuzi zaidi kibiashara. Sambamba na semina bora zitakazotolewa kwa wanawake wote ambao watapata elimu itakayotolewa wataalamu wa fani mbalimbali  
Kwa miaka mitatu mfululizo TWENDE imekuwa ikitoa fursa kwa wanawake wajasiriamali kukutana pamoja na kujadili mafanikio na changamoto ambazo zimekuwa ni kikwazo cha wanawake wajasiriamali kutofikia malengo yao kibiashara.

“Licha ya kwamba wanawake wengi wamejikita katika sekta hii ya ujasiriamali, lakini bado wamekuwa wakikabiliawa na changamoto mbalimbali zinazokwamisha kufikia malengo yao, ikiwemo elimu ya ujasiriamli na upatikanaji wa mikopo, kwa hiyo ipo haja kwa wanawake kujijengea utaratibu wa kushiriki katika fursa kama hizi zinazowajengea uwezo”. Alisema Saphia Ngalapi Meneja Mradi wa TWENDE.
Zaidi ya Wanawake Wajasiriamali Wanawake 100 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani wanatarajai kushiriki katika TWENDE mwaka huu, ampabo maonesho hayo yanakwenda sambamba na semina zitakazo tolewa kwa wanawake wote bure, kwa wale watakaoshiriki katika maonesho, na hata wale ambo watakuwa hawakupata frusa ya kuonesha na kuuza bidhaa zao.
 KUHUSU TWENDE
Tanzania Women Entrepreneurs & Networking Development Exposition (TWENDE) inapanga kuleta maendeleo kwa wanawake wajasiriamali kwa kuandaa jukwaa ambalo litakua mahususi kuweza kukutana zaidi ya wanawake wafanyabiashara 100 wadogo, wakati na wakubwa kutoka viwanda vikubwa na vidogo, taasisi za serikali na mashirika yasio ya kiserikali (NGO).
Tanzania Women Entrepreneurs & Networking Development Exposition (TWENDE) pia inalenga kuyapa fursa makampuni kukutana yakikidhi malengo ya wahudhuriaji. Ni sehemu ya kuuza na kuonyesha bidhaa na huduma za kampuni mbalimbali kwa wafanya maamuzi. Maonyesho haya yataenda sambamba na mkutano wa siku tatu utakaotoa elimu bora kwa washiriki. Kwa habari zaidi tembelea www.twende.info

0 comments:

 
Top