Tanzania Human Rights Defenders Coalition [THRD-Coalition]
Watetezi wa haki za Binadamu chini ya Mwamvuli wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu
Tanzania (THRDs),1 kwa ushirikiano na wadau wengine tunapinga vikali kufungiwa kwa gazeti la
MwanaHalisi na Serikali mnamo tarehe 30th Julai 2012 kwa kutumia Sheria ya Magazeti ya mwaka
1976 Sura ya 229. Tunatambua kwamba Mwanahalisi ni gazeti la kujitegemea na la kichunguzi hapa
Tanzania.
Kwa pamoja, tumeona kuwa kufungiwa kwa Gazeti hili kunaonesha dhahiri nia ya serikali kuleta hofu na
kuwanyamazisha wapigania haki za binadamu, vyombo vya habari, na watetezi wa haki za binadamu.
Gazeti hili la MwanaHalisi limekuwa likitoa taarifa kwa umma kuhusu nani wahusika kwenye sakata la
kutoweka na kuteswa kwa Dr Ulimboka, baada ya kuona serikali imelifumbia macho swala hili
Mwahalisi limekuwa likifanya taarifa za kichunguzi ambazo zimekuwa zikitolewa kwenye mfululizo wa
matoleo ya magazeti ya Mwanahalisi.
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDs) tumeguswa na swala hili na tumeona kuwa hii ni
nia dhahiri ya Serikali kuvizuia vyombo vingine kutokuzungumzia masuala nyeti yenye maslahi ya umma
Tunahofia kuiona Serikali inatumia sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 Sura ya 229, ambayo ni moja ya
sheria mbovu na isiyo na misingi ya haki za binadamu. Sheria hii kwa miaka mingi imekuwa ikipigiwa
kelele na ni sheria kandamizi, pia na ni sheria ambayo inapingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Achilia mbali kuwepo kwa Mikataba ya kimataifa na Katiba ya nchi yetu ambayo inatoa uhuru wa maoni
ila bado serikali yetu imejifanya haioni ni vyema kutoa uhuru wa habari. Sheria tajwa hapo juu humpa
Mamlaka mtu binafsi (Waziri) ikiwa anaona inafaa kutoa maamuzi ya kufungia Gazeti lolote kama ataona
1 The host Legal and Human Rights Centre, the Media Council of Tanzania, Media Institute of Southern Africa Tanzania
chapter, and HaliHalisi representatives, Tanzania Editors Forum, Tanzania Women Lawyers Association, and
Journalists for Human Rights.
ni kwa manufaa ya umma au kwa manufaa ya amani ya jamii. Sheria inamruhusu Waziri kufanya kazi za uhariri mkuu muda huo huo kufanya kazi za mlalamishi, mwendesha mashitaka, na kufanya kazi za Jaji. Hii ni kinyume na utawala wa sheria na kanuni za haki asli.Mfano katika tukio hili, misingi ya kanuni ya haki asili kam vile haki ya kusikilizwa, haki ya kukata rufaa na haki ya kusikilizwa na chombo kisichokuwa na maslahi yoyote katika shauri.
Kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi hakuishii kuvunja tu uhuru wa vyombo vya habari bali pia kunavunja haki ya kupata habari kama inavyotolewa na Ibara ya 19 ya Mkataba wa Haki za kijamii na Kisiasa wa mwaka 1966 (ICCPR), Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu 1981. Kifungu cha 18 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 kinatoa uhuru wa Maoni bila kikwazo cha aina yoyote.
Kwa kitendo hiki mamilioni ya Watanzania watakuwa wamenyimwa haki ya kupata taarifa na hivyo inapunguza uwajibikaji wa viongozi wa serikali. Mtandao wa THRDs pamoja na wadau wengine tunawaomba watanzania wote na wengine wenye mapenzi mema kufanya yafuatayo;
a) Serikali
i) Kuacha kuitumia hiyo sheria kandamizi ya Magazeti ya Mwaka 1976 kwa kusudi la kunyima uhuru wa maoni na taarifa.
ii) Kuipitia upya sheria hiyo na kuifanyia marekebisho
iii) Kulifungulia Gazeti la Mwanahalisi mara moja kwa lengo la kuwapa Watanzania taarifa
iv) Viongozi na maofisa wa serikali ambao wako kwenye vyombo nyeti vya serikali kufuata maadili ya kazi, na bila kutumiwa.
b) Tasnia ya Habari
i) Kuvunja ukimya na kuonesha umoja wao katika suala hili, kwani kuumia kwa mmoja ni kuumia kwa wote.
ii) Kuendelea kutafuta na kutoa taarifa zote zenye tija na maslahi kwa umma.
iii) Kuwagundua na kuwataja waandishi wa habari wanaosaliti taaluma ya habari kwa malengo yao binafsi. Na pia kuwataka waendelee kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili na weledi wa tasnia ya habari.
c) Asasi za Kiraia.
i) Kuwa na umoja pale mtetezi wa haki za Binadamu anapopata matatizo bila ya woga.
d) Umoja wa Mataifa
Umoja wa Mataifa(UN) mawakala wake, balozi mbali mbali Tanzania na asasi zote za kikanda na za kimataifa tunawaomba kuchukua hatua katika suala hili na matukio mengine yanayowaandama watetezi wa haki za binadamu Tanzania.
e) Taasisi za kidini
Kuelewa ya kuwa Taasisi za kidini, watetezi wa haki za binadamu, wanahabari, na asasi za kiraia kwa pamoja wanapingana na rushwa, ukiukwaji wa haki na utendaji mbovu wa serikali. Hivyo basi kufungiwa kwa moja kati ya hao ni tishio na ni kinyume na misingi ya dini zote. Hivyo tunawaomba umoja wao katika hili.
f) Kwa umma
Kwa kuwa umma ndiyo watu wa kwanza kupokea taarifa za vyombo vya habari, na MwanaHalisi ikiwa moja ya gazeti la kipekee la habari za kiuchunguzi, tunawaomba kuungana nasi pamoja na wadau wengine kupinga tukio hili la kufungiwa kwa gazeti.Tuwaombe wananchi kuitaka serikali kulifungulia gazeti hili na kuifanyia mabadiliko sheria hii kandamizi.
Hili tamko la pamoja limetolewa na kusainiwa leo tarehe 2 julai, 2012 na asasi, wadau mbali mbali na watetezi wa haki za binadamu kutokana na kufungiwa kwa Gazeti la MwanaHalisi na vitisho vinavyowapata watetezi wa haki za binadamu nchini.
Imesainiwa kwa niaba ya asasi na wadau mbalimbali wanaonekana katika orodha hii na;
Dr Helen Kijo-Bisimba
Mkurugenzi Mtendaji Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu
Onesmo Olengurumwa
Mratibu Mtndao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania
ORODHA YA WADAU
1. Kituo cha sheria na Haki za Binadamu - LHRC
2. Haki Madini-Arusha
3. SAHRINGON
4. Chama cha Wanasheria wa Mazingira -LEAT
5. Chama cha Wanasheria Wanawake -TAWLA
6. Kituo cha Msaada wa Sheria Zanzibar  -ZLSC
7. Asasi ya Habari ya Africa kusini mwa Af-rica -MISA-Tan
8. Chama cha Wanasheria wanawake Zanzibar -ZAFELA
9. Jukwaaa la Jamii ya Wafugaji Tanzania -TPCF
10. Waandishi wa Habari wa Haki za Bi-nadamu-TAMWA
11. PAICODEO- Morogogoro
12. TUFAE-Songea
13. MVUHA – Shinyanga
14. CHAUMTA- Geita
15. MFUMA--Shinyanga
16. JAWAWAVI – Rukwa
17. SNDF- Shinyanga
18. Chama cha Maalbino Tanzania - TAS
19. Jukwaa la Wahariri -TEF
20. Baraza la Habari Tanzania -MCT
21. Jumuiya ya Elimu ya Haki za Binadamu na Amani- Mbeya
22. PINGOS Forum-

0 comments:

 
Top