Jamuhuri ya Watu wa China imeahidi kuendelea kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika harakati zake za Maendeleo , Uchumi na hata Maafa na Majanga wakati  yanapotokea.Wito huo umetolewa na Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Bibi Sheen Limun wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyekwenda kumpa pole kufutia maafa ya ajali ya Meli ya M.V Skagit iliyotokea Jumanne iliyopita karibu na Kisiwa cha Chumbe.
Balozi Sheene aliambatana na Uongozi wa Kampuni za Ujenzi za China zinazofanya kazi hapa Zanzibar za Railway Jiangchang Engineering Co Ltd na ile ya Beijing Construction Engineering Group ambazo zote zimekabidhi mchango wa shilingi milioni tano kila moja kusaidia Mchango wa Maafa hafla iliyofanyika katika Ofisi ya Spika wa Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar .
 Alisema Wananchi wa Jamuhuri ya Watu wa China wanajua hali ya huzuni iliyoikumba Jamii ya Watanzania hasa wazanzibari kutokana na msiba huo wa kuzama kwa Meli iliyosababiha vifo vya wananchi waliyomo kwenye boti hiyo. 
                                                                                                                                    Balozi  Sheen alimhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwamba ushirikiano wa wa kihistoria  kati ya pande hizo mbili utaendelea kudumishwa kwa hatma ya Nchi hizo mbili.
Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliipongeza Serikali ya Jamuhuri ya Watu wa China kupitia Balozi zake Nchini Tanzania kwa jitihada zake za kuunga mkono Harakati za  Maendeleo hapa Nchini. 
 Balozi Seif alimueleza Balozi Mdogo wa China Aliyepo Hapa Zanzbar kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeanza kuchukuwa hatua mbali mbali za kujihami au kuwepuka Maafa wakati yanapotokezea Majanga.  
 Alisema Serikali kupitia ushirikiano wa pamoja wa Mamlaka za Usafiri wa Baharini za Bara { Sumatra} na ile ya Zanzibar { ZMA } zitawajibika kuvifanyia uchunguzi vyombo vyote vya usafiri wa Baharini kila muda kwa vile vitavyoruhusiwa kutoa huduma hiyo
“ Wamiliki wa Vyomo vya Usafiri wa Baharini lazima wafuate sheria na Taratibu za Mamlaka ya usafiri wa Baharini kwa lengo la kuwepuka maafa yanayoweza kukingika”. Alisisitiza Balozi  Seif
Aidha Balozi Seif aliongeza kwamba taratibu zitaendelea kuimarishwa  ili kuona Mwekezaji anayeagiza vyombo vya Usafiri wa Baharini anawasilisha vielelezo vyake vya chombo husika kwanza kabla ya kuagiza ili kufanyia uhakiki wa kitaalamu
Wakati huo huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alikutana naMkurugenzi anayeshughulikia Masuala ya Afrika na Carribean wa Umoja wa Ulaya { EU } Bibi Fransisca Mosca hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar
Katika mazungumzo yao Balozi Seif aliuomba Umoja huo wa Ulaya kuangalia uwezekano wa kusaidia juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar za kutafuta mbinu za upatikanji wa usafiri wa uhakika kati ya Unguja na Pemba.                                        
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakudia kuwa na Meli zake kama kawaida baada ya zile zilizokuwa zikutumika kupitwa na muda wake wa matumizi
Naye Mkurugenzi huyo anayeshughulikia masuala ya Afrika na Carribean Bibi Fransisca Mosca alimuhakikishia Balozi Seif kwamba ushirikiano wa muda mrfu uliopo kati ya Umoja huo na Zanzibar na Tanzania kwa ujumla utaendelezwa.
Othman Khamis Ame                               
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar 

0 comments:

 
Top