Tunavyoshuhudia viwanda katika bara hili viking'ang'ana kutengeneza na kusambaza umeme unaotosha kufikia kiwango msingi, usambazaji unaonekana kuwa changamoto kubwa zaidi kwa ufikiaji wa umeme barani Afrika.

Kwa sasa, kuna viwango vya uwekezaji ambavyo havijawahi kuonekana katika sekta ya uzalishaji umeme- haikaribii tu utafutaji tena. Wawekezaji leo wanaona uzalishaji umeme kama fursa iliyotajwa na watu wengine kuwa kubwa kiasi kwamba itafanya mapato ya makampuni makubwa ya simu barani Afrika yaonekane kuwa madogo.

Hata hivyo, licha ya zaidi ya dola bilioni 8 za Marekani kuwekezwa katika miradi mipya nchini Afrika Kusini peke yake, usambazaji unaendelea kuporomoka, huku ukiathiri hali ya kijamii na siasa katika bara la Afrika pakubwa. Zaid ya hayo, jambo hili linatishia uthabiti wa miradi ya uzalishaji wa siku zijazo ambayo tayari inaendelea kujengwa.

Baada ya zaidi ya miaka 20 ya ujenzi, EAPP, SAPP, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Benki ya Maendeleo ya China na Benki ya Dunia pamoja na wabia wa sekta ya umma nchini Uhabeshi, Kenya, Zambia, Tanzania, Msumbiji, Zimbabwe na Afrika Kusini zinaanza kuonyesha mafanikio ambayo hatimaye yanaweza kuwa mwisho wa matatizo ya usambazaji.

Miradi hii inaweza kuwa mwanzo wa fursa za ajabu kwa Afrika Mashariki na Kusini, ikikuza kila kitu kuanzia usambazaji wa umeme katika miji hadi ukuaji wa viwanda. Matokeo haya yatapatikana tu ikiwa nchi hizi zinaweza kutumia hadi upeo uwezo wa watengenezaji na watasinia wanaoepuka kwa hali wakitafuta kunufaika na kanda za uhamishaji ambazo zinaendelea kukua kwa sasa.

Unafaa kuona tu kile Umoja wa Falme za Kiarabu zimetimiza ili uone vile uchumi unaotegemea rasilimali unaweza kubadilisha utajiri wa nchi ikiwa uwekezaji unaofaa katika muundo msingi unafanywa. Kwa upande mwingine, kuna mifano ambapo uwekezaji huu muhimu haukufanywa - na basi kusababisha ghasia za kijamii.

Swali basi ni hili - ni rais yupi atakabiliana na changamoto hii na aunde urithi kwenye bara hili unaosoma, "Nilileta umeme barani Afrika, nilileta mabadiliko?"

EnergyNet, kama ilivyokuwa ikifanya kwa miaka 17 iliyopita, itarahisisha majadiliano haya kwa kukaribisha waamuzi 100 muhimu nchini Kenya kuanzia tarehe 25-27 Machi kwa mkutano wa Kusambaza Umeme Afrika Mashariki. DFI kuu, waendelezaji uzalishaji wa umeme na makampuni ya usambazaji yatakuja pamoja ili kushawishi mazungumzo, wakiwezesha washiriki kuelewa kinachoendelea katika mtandao wa usambazaji wa Afrika Mashariki kati ya muda mfupi na muda mrefu.

Distributed by APO (African Press Organization) on behalf of EnergyNet Ltd.

0 comments:

 
Top