Mw.Peik Johansson akimfamisha mshiriki wa
mafunzo ya kutengeneza blog Nd.Ramadhani
kutoka katika gazeti la Zanzibar Leo

ikiwa ni siku ya tatu tangu mafunzo kwa waandishi wa habari yahusuyo blog, yakiwa yanaendelea, waandishi au washiriki katika mafunzo hayo wameweza kufikia hatua kubwa kwa vile kila mtu ameweza kutengeza blog yake mwenyewe

hata hivyo, katika siku hii ya tatu hatua kubwa ambayo ilifikiwa ikiwa ni pamoja na kuzifanyia masahihisho habari zilizo ingizwa kwenye blog pamoja na kuzitembelea web site tofauti ikiwa ni pamoja na kuangalia Idadi ya watu katika mji wa RUVUMA, EGPTY, BUKINA FASO,BOLIVIA, FINLAND n.k
aidha, washiriki pia waliweza kuangalia na kutafuta taarifa za Rais wa Bolivia Evo Morales, ikiwa ni pamoja na kujuwa historia yake kwa ufupi, majirani wa Bolivia pamoja na sera za nje za Rais Evo Morales.
mbali na hayo, washiriki wa mafunzo wamatakiwa kuwa makini na kuweza kuwafundisha wenzano wakati watakapo rudi katika taasisi zao

0 comments:

 
Top